Wachezaji wa soka wagoma kurudi uwanjani

Iliyochapishwa

Meneja wa timu ndogo nchini Uingereza ya Abingdon amejiuzulu baada ya wachezaji wake kugoma kurudi uwanjani kwa kipindi cha pili cha mchezo kwani tayari walikuwa wameshapokea kichapo cha magoli 8 bila jibu. Meneja wa klabu hiyo Tranell Richardson amesema aliunga mkono uamuzi huo wa wachaaji wake kwani hawakutaka adhabu zaidi.