Kwanini gharama ya Uchaguzi Kenya iko juu duniani?
Kwanini gharama ya Uchaguzi Kenya iko juu duniani?
Iliyochapishwa
Kenya inatazamiwa kuendesha moja ya chaguzi ghali zaidi duniani tarehe 9 Agosti mwaka huu .
Uchaguzi huo unaotarajiwa kugharimu $3 bilioni katika matumizi ya jumla unatarajiwa kuwa ghali zaidi barani Afrika kwa msingi wa gharama kwa kila mpiga kura.
Matumizi ya umma na ya kibinafsi yamefikia kiwango cha juu kabisa, huku serikali na wagombea wakitumia mamia ya mamilioni ya dola kupata mchakato wa uchaguzi au kufanya kampeni ili kuchaguliwa.




