Viktor Bout: Je Mfanyabiashara wa mauti ni nani?

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mamlaka ya Urusi imetaka Bw. Bout arejeshwe tangu kuhukumiwa kwake 2011.
Iliyochapishwa

 

Viktor Bout, mmoja wa wafanyabiashara maarufu wa silaha duniani, ameachiliwa kutoka chini ya ulinzi wa Marekani kama sehemu ya kubadilishana wafungwa na nyota wa mpira wa vikapu wa Marekani Brittney Griner.

Griner alikuwa kizuizini tangu Februari baada ya maafisa wa uwanja wa ndege wa Moscow kupata mafuta ya bangi kwenye mzigo wake alipokuwa akirejea Marekani baada ya kucheza nchini Urusi.

Uvumi ulikuwa umeenea katika vyombo vya habari vya Marekani kwa miezi kadhaa kwamba maafisa wakuu wa idara ya serikali walikuwa wakitaka kupata kuachiliwa kwa Griner ili kubadilishana na uhuru wa mfanyabiashara huyo wa silaha.

Ushujaa wa afisa huyo wa zamani wa jeshi la anga la Soviet ni maarufu sana hivi kwamba ulichochea filamu ya Hollywood, na wakampatia jina la utani la kutisha.

Lakini ni nani mtu huyu anayejulikana kuwa Mfanyabiashara wa Mauti?

Bout alirejeshwa kutoka Thailand hadi Marekani mwaka 2010, baada ya operesheni kali ya Shirika la Kupambana na Dawa za Kulevya nchini Marekani (DEA) miaka miwili iliyopita.

Mawakala kutoka DEA walijifanya kuwa wanunuzi kutoka kwa Wanajeshi wa Mapinduzi wa Colombia, wanaojulikana kama Farc. Kundi - ambalo limesambaratika - liliorodheshwa kama shirika la kigaidi na Marekani.

 Bout alidai kuwa alikuwa mfanyabiashara mwenye biashara halali ya usafiri wa kimataifa, akishutumiwa kimakosa kwa kujaribu kuwapa silaha waasi wa Amerika Kusini - wahanga wa njama za kisiasa za Marekani.

Lakini jopo la mahakama huko New York halikuamini simulizi yake.

Alihukumiwa kifungo cha miaka 25 jela mwezi Aprili 2012 baada ya kupatikana na hatia ya kula njama ya kuwaua Wamarekani na maafisa wa Marekani, kusambaza makombora ya kutungulia ndege na kusaidia shirika la kigaidi.

Kesi yake ya wiki tatu ilisikia kuwa Bout aliambiwa kuwa silaha hizo zingetumika kuwaua marubani wa Marekani wanaofanya kazi na maafisa wa Colombia. Waendesha mashtaka walisema alijibu: "Tuna adui sawa."

Bout - raia wa Urusi aliyezaliwa katika Tajikistan iliyotawaliwa na Soviet - alianza kazi yake ya usafiri wa anga mapema miaka ya 1990, baada ya kuanguka kwa USSR.

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Viktor Bout alitumikia zaidi ya miaka miwili katika jela ya Bangkok.
Hauhitaji Whatsapp
BBC Swahili sasa kwenye WhatsApp

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Bonyeza hapa kujiunga

Mwisho wa Whatsapp

Bout alirejeshwa kutoka Thailand hadi Marekani baada ya juhudi za wanadiplomasia wa Urusi kumtaka aachiliwe kushindikana.

Antonovs na Ilyushins imara zilikuwa zikiuzwa pamoja na wafanyakazi wao, na zilikuwa bora kwa ajili ya kupeleka bidhaa kwenye viwanja vya ndege vya wakati wa vita duniani kote.

Bout - ambaye alikuwa na umri wa miaka 45 alipohukumiwa - anasemekana alianza kusambaza silaha kupitia msururu wa makampuni ya juu katika maeneo yenye vita barani Afrika.

Umoja wa Mataifa ulimtaja kama mshirika wa Rais wa zamani wa Liberia Charles Taylor - ambaye alipatikana na hatia mwaka 2012 kwa tuhuma za kusaidia uhalifu wa kivita wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Sierra Leone.

"[Bout ni] mfanyabiashara, muuzaji na msafirishaji wa silaha na madini [ambaye] aliunga mkono utawala wa Rais wa zamani Taylor katika [jitihada] za kuvuruga Sierra Leone na kupata ufikiaji haramu wa almasi," nyaraka za Umoja wa Mataifa zinaeleza.

Vyombo vya habari katika Mashariki ya Kati vilidai kuwa alikuwa mtoro wa al-Qaeda na Taliban.

Pia anadaiwa kuzipa silaha pande zote mbili katika vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Angola na kusambaza silaha kwa wababe wa kivita na serikali kutoka Jamhuri ya Afrika ya Kati na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa Sudan na Libya.

Katika mahojiano na Channel 4 News ya Uingereza mwaka 2009, alikanusha katakata kuwahi kushirikiana na al-Qaeda au Taliban.

Lakini alikiri kupeleka silaha hadi Afghanistan katikati ya miaka ya 1990, akisema zilitumiwa na makamanda wanaopigana dhidi ya Taliban.

Pia alidai kuwa aliisaidia serikali ya Ufaransa kusafirisha bidhaa hadi Rwanda baada ya mauaji ya kimbari, na kuwasafirisha walinda amani wa Umoja wa Mataifa.

Lakini vyombo vya kutekeleza sheria vilimfuata katika miaka ya 2000. Aliondoka nyumbani kwake Ubelgiji mwaka 2002 wakati mamlaka huko ilipotoa kibali cha kukamatwa.

Inafikiriwa Bout alisafiri chini ya majina kadhaa, akipitia nchi kama vile Falme za Kiarabu na Afrika Kusini kabla ya kuibuka tena nchini Urusi mnamo 2003.

Katika mwaka huo huo, waziri wa mambo ya nje wa Uingereza Peter Hain alimpa jina la utani la Merchant of Death

Baada ya kusoma ripoti ya 2003 kumhusu, Bw Hain alisema: "Bout ndiye mfanyabiashara mkuu wa mauti ambaye ndiye mfereji mkuu wa ndege na njia za usambazaji wa silaha ... kutoka Ulaya Mashariki, haswa Bulgaria, Moldova na Ukraine hadi Liberia na Angola. .

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Bout alirejeshwa kutoka Thailand hadi Marekani baada ya juhudi za wanadiplomasia wa Urusi kumtaka aachiliwe kushindikana.

Mamlaka ya Urusi imetaka Bw. Bout arejeshwe tangu kuhukumiwa kwake 2011.

Marekani ilifanya harakati dhidi ya Bout katika miaka ya 2000, na kufungia mali yake mwaka wa 2006, lakini hakukuwa na sheria ambayo angeweza kufunguliwa mashtaka nchini Marekani.

Badala yake, maajenti wa Marekani waliomba muda wao hadi 2008 walipojifanya wanunuzi wa waasi wa Farc wa Colombia na kupata utambulisho wa Bout kupitia kwa washirika wake wa zamani.

Muda mfupi baada ya maafisa wa siri kujadili usafirishaji wa silaha kwenda Farc na Bout, mamlaka ya Thailand ilimkamata na kesi ndefu za kisheria zilianza kumleta Marekani.

Bout alisema kesi ya Marekani dhidi yake ilichochewa kisiasa; mkewe amenukuliwa akisema uhusiano wake pekee na Colombia ulikuwa "mafunzo ya tango".

Mamlaka ya Urusi ilimuunga mkono wakati wote wa kesi zake za kisheria, huku Waziri wa Mambo ya Nje Sergei Lavrov akiapa kupigana ili kupata kurejea kwake Urusi na kuandika uamuzi wa mahakama ya Thailand "usio wa haki na wa kisiasa".

Filamu ya 2005 ya Lord of War, iliyoangazia maisha ya muuza silaha huyo, ina shujaa anayeepuka haki mwishoni.

Lakini mwisho kama huo ulimkwepa Bout, ambaye alikuwa amebaki gerezani nchini Marekani tangu kuhukumiwa kwake mwaka 2012.