Urafiki au kujiimarisha: Kwanini Xi Jinping anazuru Korea Kaskazini?

(L-R) Rais wa Urusi Vladimir Putin akitembea na Rais wa China Xi Jinping na Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Xi na Kim walikutana mara ya mwishi mwezi Septemba mjini Beijing kwenye gwaride la kijeshi
    • Author, Laura Bicker
    • Nafasi, Mwandishi wa China
  • Iliyochapishwa
  • Muda wa kusoma: Dakika 6

Kwa kiongozi wa China Xi Jinping, Korea Kaskazini ni jirani ambaye China haiwezi kumdhibiti wala kudhubutu kumpoteza.

Pande hizo mbili mara nyingi huelezea uhusiano wao kama "uliotokana umwagikaji wa damu", kumbukumbu ya Vita vya Korea.

Lakini katika miaka ya hivi karibuni, kutoaminiana kumezorotesha uhusiano huo. Na sasa Beijing inajaribu tena kuhuisha uhusiano na mshirika huyu muhimu wa kimkakati lakini asiyetabirika.

China inataka utulivu kwenye mpaka wake na ushawishi huko Pyongyang, lakini bila kuingizwa katika migogoro iliyochochewa na malengo ya nyuklia ya Korea Kaskazini.

Kwa hivyo ziara ya Xi wiki hii huenda isiwe ya kiurafiki vela bali kuhusu kujiimarisha.

Seoul anaamini kuwa anaweza kumtumia China kama mpatanishi kati ya Korea Kaskazini na Marekani, lakini Beijing huenda ina nia nyingine.

Duru za kidiplomasia za nchi za Magharibi zinaiambia BBC kwamba China imezidi kuwa na wasiwasi kuhusu kuongezeka kwa ushirikiano kati ya Pyongyang na Moscow.

Baada ya kukutana na Rais wa Urusi Vladimir Putin wiki iliyopita, huenda Xi akataka kuhakikisha pia anamdhibiti kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un, hasa wakati Beijing ikiongeza uwepo wake katika jukwaa la kimataifa.

kuimarisha uhusiano unaoyumba

Hauhitaji Whatsapp
BBC Swahili sasa kwenye WhatsApp

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Bonyeza hapa kujiunga

Mwisho wa Whatsapp

Mvutano kati ya Beijing na Pyongyang ulionekana, hata kama ulikuwa wa hila.

Hawakuadhimisha miaka 75 ya uhusiano wa kidiplomasia mnamo Oktoba 2024.

Balozi wa China hakuhudhuria sherehe za kuanzishwa kwa Korea Kaskazini mwezi uliopita. Hakukuwa na mawasiliano ya ngazi ya juu kwa kipindi cha mwaka mzima, tofauti kabisa na uhusiano wa usuhuba kati ya Pyongyang na Moscow.

Ukaribu huo na Urusi unaoendelea kushamiri unaonekana kuikosesha Beijing usingizi.

Baada ya uvamizi wa Urusi nchini Ukraine, Korea Kaskazini imepanua ushirikiano wa kijeshi na Putin, na kilele chake imekuwa makubaliano ya ulinzi wa pande zote ambayo yalitiwa saini wakati wa ziara ya Putin huko Pyongyang mnamo 2024.

Takriban wanajeshi 2,300 wa Korea Kaskazini wamefariki wakipigania Urusi nchini Ukraine, kulingana na uchunguzi wa BBC. Pyongyang pia inashutumiwa kwa kutoa silaha kusaidia juhudi za vita za Urusi badala ya mafuta na misaada, jambo ambalo limeitia wasiwasi Washington na washirika wake, na kuishinikiza China kimya kimya.

"China inataka kuhakikisha kwamba maslahi yake dhidi ya Korea Kaskazini yanalindwa katika ushirikiano kati ya Moscow na Pyongyang," anaongeza Ankit Panda, mtaalamu wa sera za nyuklia katika Shirika la Carnegie kwa Amani ya Kimataifa.

Pedestrians walk past a mural (L) that reads "For the safety and endless future of our nation", as a building adorned with the slogan "Long live the great people-first politics" is seen in the background in Pyongyang on May 8, 2026.

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

Maelezo ya picha, Kwa kuwa Korea Kaskazini imetengwa na ulimwengu, utawala wa kidikteta wa nchi hiyo unategemea sana China na Urusi

China ina mkataba mmoja rasmi wa ulinzi na Korea Kaskazini.

Kwa hivyo Beijing haingelitaka kutoa na fasi kwa Urusi kuimarisha ushawishi wake huko Pyongyang. Kim anayejiamini zaidi, asiyetegemea sana atapunguza uwezo wa Wachina.

Beijing imejibu kufumbua kitendawili hiki kwa kujaribu kufufua upya uhusiano huo. Mwishoni mwa mwaka jana, Xi alimwalika Kim kwenye gwaride la kijeshi huko Beijing, akimuweka kando yake pamoja na Putin.

Ulikuwa mkutano wao wa kwanza rasmi katika kipindi cha miaka sita. Xi aliwasifu wawili hao kama "majirani wema, marafiki wazuri na ndugu wazuri wanaofungamana na hatima ya pamoja", na kutoa wito wa uratibu wa kimkakati wa karibu zaidi. Kinachokosekana katika taarifa za umma ni kutajwa kwa silaha za nyuklia za Korea Kaskazini.

Beijing ina "mchanganyiko wa hisia" kuhusu ushirikiano unaokua kati ya Pyongyang na Moscow, anasema Lee Seong-hyon, mtaalamu katika Kituo cha Asia cha Chuo Kikuu cha Harvard.

Kwa upande mmoja, ushirikiano huo "unaivuruga Washington na kutatiza mkakati wa Marekani katika kumbi nyingi za sinema, ambazo zinanufaisha China kwa njia isiyo ya moja kwa moja," Lee anasema.

Lakini, anaongeza, kupanua ushirikiano wa kijeshi kati ya Urusi na Korea Kaskazini kunaweza kuibua mwitikio mkubwa wa kijeshi wa pande tatu kutoka kwa Marekani, Japan na Korea Kusini, jambo ambalo litaitia wasiwasi Beijing.

Ndio maana pia China haiungi mkono mpango wa nyuklia wa Pyongyang - kwa sababu hiyo itaongeza ushiriki wa Marekani katika eneo na ushirikiano wake hapa.

Lakini pia China haikabiliani na suala hilo moja kwa moja. Mwaka 2022, China na Urusi zilipinga azimio la Umoja wa Mataifa lililoongozwa na Marekani la kuweka vikwazo vipya kuhusu majaribio ya makombora ya Korea Kaskazini.

Endapo China itachukua msimamo mkali dhidi ya mpango wa nyuklia wa Pyongyang, "hii itaisukuma Korea Kaskazini zaidi kwenye mikono ya Putin," anasema Victor Cha, rais wa idara ya sera za kigeni katika Kituo cha Mafunzo ya Kimkakati na Kimataifa.

Mshirika mwenye mtazamo chanya

Lakini Kim hana nia ya kutenganisha chanzo chake kikubwa cha misaada pia.

Mauzo ya China kwa Korea Kaskazini yaliongezeka hadi karibu dola bilioni 2.3 za Kimarekani mwaka jana, kiwango cha juu zaidi katika kipindi cha miaka sita. Huduma za treni za abiria kati ya Beijing na Pyongyang zilianza tena mapema mwaka huu baada ya kusimamishwa kwa miaka sita.

Wachambuzi wanasema hii pia ni juhudi iliyokadiriwa na Beijing kuirudisha Pyongyang kwenye upeo wake.

Kwa Kim, ni chaguo la kisayansi. Ikiwa vita vya Ukraine vitaisha, hitaji la Urusi la kuungwa mkono na Korea Kaskazini linaweza kupungua. Na tofauti na Putin aliyejitenga, Xi amekuwa akiwakaribisha viongozi wa dunia mjini Beijing.

Hivyo Kim anatakiwa kuhakikisha haachiwi kumtegemea mpenzi aliyedhoofika.

North Korean leader Kim Jong Un (C) and his daughter Ju Ae (L) responding to citizens

Chanzo cha picha, Getty via KCNA

Maelezo ya picha, Mara nyingi Kim Jong Un ameonekana hadharani akiwa na binti yake Kim Ju Ae - baadhi ya wachunguzi wanaamini kuwa huenda akawa mrithi wake

Lakini uhusiano huu ulikumbwa na changamoto kuanza mwanzo.

Kim aliingia madarakani akiwa na vipaumbele vilivyotofautiana na baba yake. Wakati Kim Jong Il alitembelea China mara kwa mara na kutegemea uungwaji mkono wa Beijing, mtoto wake alichukua hatua haraka kufanikisha mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini. Katika miaka yake sita ya kwanza madarakani, Kim alisimamia takribani majaribio 90 ya makombora ya balestiki na majaribio manne ya makombora ya nyuklia - ukilinganisha na baba yake na babu yake kwa pamoja.

Hii ilitia wasiwasi Beijing. Kunyongwa kwa mjomba wa Kim, Jang Song Thaek, aliyeonekana na hinCa kama mtu mwenye utulivu, kulizidisha mpasuko.

Xi alijibu kwa ishara nadra za kidiplomasia za kutoridhishwa, akizuru Korea Kusini mnamo 2014 kabla ya kukutana na Kim: hatua ambayo ilitafsiriwa na wengi kama chuki.

Korea Kaskazini ilijibu kwa kuita China "adui yetu."

Ni hadi mwaka 2018, wakati athari ya vikwazo dhidi mpango wake wa nyuklia ilipoanza kusikika, ambapo Kim alifanya ziara yake ya kwanza ya nje ya nchi.

Alipanda treni yake ya kivita na kuelekea Beijing. Mkutano huo uliashiria kuanza kwa ufufuaji wa uhusiano wao kwa uangalifu.

Kim angeenda kukutana na viongozi wa Marekani na Korea Kusini, lakini ilikuwa mara kwa mara baada ya kushauriana na China. Ujumbe ulikuwa wazi: Pyongyang haitafanya mazungumzo bila kuungwa mkono na Beijing.

Leo, Korea Kaskazini inatumika kama uzio na mzigo kwa China. Inaviweka vikosi vya Marekani kwa urefu, lakini majaribio yake ya silaha yanavuruga eneo hilo.

Wakati huo huo, Kim anataka ulinzi wa Wachina - bila udhibiti wa Wachina.

Hakuna upande unaomwamini mwingine kikamilifu. Lakini kwa sasa, wote wawili wanaamini kuwa wanahitaji mwingine na hiyo inatosha kuwafanya wazungumze.

Ripoti ya ziada ya Kelly Ng