Man Utd itabidi ifanye uamuzi juu ya Fernandes - Tetesi za soka Ulaya Jumamosi

.

Chanzo cha picha, Reuters

Iliyochapishwa
Muda wa kusoma: Dakika 3

Vilabu kutoka Saudi Arabia na Ulaya vinatazamiwa kuijaribu nia ya Manchester United kuendelea kumshikilia nahodha Bruno Fernandes mwezi Januari, Napoli wanaongoza katika mbio za kumsajili kiungo wa kati wa Manchester United Kobbie Mainoo, huku Barcelona na Liverpool wakimtaka beki wa Bayern Munich Dayot Upamecano.

Azma ya Manchester United ya kumbakisha nahodha wao Bruno Fernandes, 31, inatazamiwa kuwa katika majaribu wakati wa dirisha dogo la usajili Januari huku vilabu vya Saudi Pro League na Ulaya vikimhitaji kiungo huyo wa kati wa Ureno. (Manchester Evening News)

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Napoli wako mstari wa mbele kumsajili kiungo wa kati wa Manchester United na Uingereza Kobbie Mainoo, 20, mwezi Januari. (Tuttomercatoweb - in Italian)

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Barcelona wanatazamiwa kushindana na Liverpool kumsajili beki wa Ufaransa Dayot Upamecano, 26, mkataba wake utakapokamilika Bayern Munich msimu ujao wa joto. (Fichajes in Spanish)

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Arsenal itakubali ofa ya takriban pauni milioni 30 kwa Gabriel Jesus, 28, huku Everton ikitarajiwa kumnunua mshambuliaji huyo wa Brazil mwezi Januari. (Teamtalk)

.

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

Newcastle wangependa kumrejesha kiungo wa kati wa Nottingham Forest na England Elliot Anderson, 22, katika klabu hiyo baada ya kumuuza miezi 16 iliyopita. (Mail)

Manchester City wanafuatilia hali ya beki wa kulia wa Atletico Madrid na Argentina Nahuel Molina, 27. (Teamtalk)

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Chaguo la mshambuliaji wa Liverpool Federico Chiesa lilikuwa daima kusalia Anfield msimu huu licha ya nia za klabu za nyumbani za Mtaliano huyo mwenye umri wa miaka 27. (Athletic - subscription required)

Crystal Palace wanaonyesha nia ya kumnunua kiungo mtarajiwa wa AZ Alkmaar Kees Smit, 19, ambaye ameichezea Uholanzi katika kiwango cha Under-19 na kuvutia Real Madrid, Barcelona, Chelsea na Manchester United. (Mail)

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Aliyekuwa mkufunzi wa Manchester United Erik ten Hag anaweza kurejea kwenye uongozi na kuchukua nafasi ya Mholanzi mwenzake Johnny Heitinga katika klabu ya zamani ya Ajax kufuatia kuwa Bayer Leverkusen kwa muda mfupi. (De Telegraaf via Goal)

Crystal Palace wanamtaka kiungo wa kati wa Japan Daichi Kamada, 29, kuongeza muda wake wa kukaa Selhurst Park huku mkataba wake ukikamilika msimu ujao wa joto. (Sky Sports)

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Bayern Munich ni moja ya klabu zinazomtaka beki wa Arsenal Mholanzi Jurrien Timber, 24, ambaye ameanza mazungumzo kuhusu mkataba mpya na The Gunners. (Caughtoffside)

Mkurugenzi anayekuja wa kandanda wa Newcastle Ross Wilson atakuwa na jukumu la kukagua klabu hiyo na kushughulikia kipindi cha uhamisho wa majira ya kiangazi atakapoanza jukumu lake huko St James' Park. (The I - subscription required)

Kipa wa Bayern Munich Mjerumani Manuel Neuer, 39, anafikiria kuongeza muda wake wa kucheza zaidi ya 2026 na kusaini mkataba mpya na klabu hiyo ya Bavaria. (Bild - in German)