Misa ya Papa Sudan Kusini: Papa Francis awataka raia kukataa 'sumu ya chuki'

Chanzo cha picha, AFP
Papa Francis amemaliza hija yake ya amani nchini Sudan Kusini kwa kuadhimisha misa ya wazi iliyohudhuriwa na makumi kwa maelfu mjini Juba.
Aliwataka waumini kukataa kile alichokiita "sumu ya chuki", na kuwaambia wasipoteze nafasi yoyote ya kujenga amani.
Na aliwasihi viongozi wa nchi hiyo kuzingatia kumaliza migogoro.
Kabla ya kuondoka, aliuambia umati hivi: “Ndugu na dada wapendwa, ninarudi Roma pamoja nanyi karibu zaidi na moyo wangu.
Wakatoliki waliokuwa na furaha, baadhi yao waliopiga kambi usiku kucha kwa ajili ya Misa, waliambia Reuters kuwa ulikuwa wakati wa furaha.
"Hadi sasa silali, nilifurahi sana," Jovana Buyom alisema.
"Kwa kweli tumefurahishwa sana na ujio wa Papa kwa sababu atatupa ujumbe wa amani, tunaweza kuungana kama watu wa Sudan Kusini," Juaj Bol Ayuel alisema.

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, Reuters
Misa hiyo iliyofanyika katika Kaburi la John Garang mbele ya hadhira ya watu 70,000 kulingana na makadirio, ilijaa waumini wenye furaha wakipeperusha bendera na kusali sana.
Sherehe za kidini zilifanyika siku ya mwisho ya ziara ya Papa nchini Sudan Kusini, ambayo ilikuwa ya kwanza kwake nchini humo.
Tangu ilipopata uhuru mwaka wa 2011, nchi hiyo imekumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe baada ya rais kutofautiana na makamu wake wa rais mwaka 2013.

Chanzo cha picha, AFP
Licha ya makubaliano ya amani mwaka 2018, ghasia zinazochochewa na mizozo ya kikabila zimeendelea - zaidi ya watu 400,000 wanakisiwa kufa kutokana na mzozo huo.
Takriban watu 20 waliuawa katika uvamizi wa mifugo usiku wa kuamkia ziara ya viongozi hao wa kidini.

Chanzo cha picha, Getty Images
Papa, ambaye alitembelea nchi hiyo pamoja na viongozi wengine wa Kikristo - Askofu Mkuu wa Canterbury, Justin Welby, na Msimamizi wa Mkutano Mkuu wa Kanisa la Scotland, Mchungaji Iain Greenshields - amekuwa kwenye misheni ya amani na kuwasihi makasisi wa Sudan Kusini kupaza sauti zao dhidi ya dhuluma siku ya Jumamosi.

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, Reuters
Pia aliwaambia kwamba hawawezi kubaki upande wowote dhidi ya udhalimu: "Ikiwa tunataka kuwa wachungaji wanaoombea, hatuwezi kubaki upande wowote kabla ya maumivu yanayosababishwa na vitendo vya udhalimu na unyanyasaji. Kukiuka haki za kimsingi za mwanamke au mwanamume yeyote ni kosa. dhidi ya Kristo."

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, AFP

Chanzo cha picha, Getty Images
Papa alikuwa na ujumbe sawa na huo wa amani na upatanisho alipozuru Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo mapema wiki hii.












