Matokeo ya uchaguzi Tanzania 2020: Serikali ya Tanzania yajibu madai ya vitisho dhidi ya viongozi wa upinzani

Iliyochapishwa

Serikali ya Tanzania imekana ripoti za vitisho dhidi ya viongozi wa upinzani nchini humo, baadhi yao wakiwa wamenukuliwa wakisema kwamba wamekuwa wakipokea vitisho na kuamua kutoroka nchini humo.

Msemaji wa serikali Dkt. Hassan Abbas amesema kwamba ni muhimu kwa kiongozi yeyote ambaye alikuwa ametishiwa kuwasilisha malalamishi yake kwa vyombo vya usalama.