Nini kinachoendelea Iran?

Iliyochapishwa

Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu, Amnesty International linasema kuna ripoti za kuaminika zinazoashiria kuwa watu 106 wameuawa nchini Iran tangu Ijumaa wiki iliyopita wakati wa maandamano ya kupinga ongezeko la bei ya petroli.

Umoja wa mataifa umetoa wito kwa maafisa wa usalama kutotumia nguvu kupita kiasi dhidi ya waandamanaji na kuomba huduma ya intaneti kurudishwa.