Van Gaal na Neyo walihudhuria tamasha la kuwapatia majina Sokwe Rwanda

Iliyochapishwa

Rwanda imewapa majina watoto wa sokwe 25 ikiwa ni desturi inayofanyika kila mwaka kwa ajili ya kuvutia ulimwengu kutembelea sokwe hao .

Wakati huo huo serikali ya nchi hiyo imetangaza kwamba idadi ya sokwe hao iliongezeka kwa kiwango cha asilimia 26 tangu mpango kabambe wa kuwahifadhi ulipoanza mwaka 2003.